TISA DISEMBA NA UHURU WA FIKRA


"Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa  fikra" moja ya nukuu za Hayati Mwalimu Nyerere JK. Akimaanisha umaskini unaotokana na fikra za kitumwa, kushindwa au kutopewa fursa ya maamuzi juu ya hatma yako, kuwepo duniani kwa lengo la  kuongeza idadi ya raia  na si  huru  kama wengine.

"Hakuna anayeweza kukutawala bila kuanzia kwenye ufahamu wako" utawala mzuri na makini unaanzia kwenye fahamu yani kukufanya utengeneze fikra ya kuwa mtumwa na uwe  umeridhika na kutumika. Siku  hizi neno zuri ni  Mtumishi( ina  maana sawa na mtumwa wakati mwingine lina maanisha mfuasi).

Uhuru una maana halisi ya kuwa na haki ya maamuzi binafsi bila ya kuingiliwa na mtu  au taifa lingine. Huwezi kufanya maamuzi yako bila kuhusisha fikra. Kwa maana hiyo mwenye Uhuru Wa fikra pekee ndio raia  huru  kweli na si  vinginevyo.

"Mtumwa hata akipewa haki ya kuamua atafanya kama anavyofikiri Bwana wake."

Uhuru tulionao unatakiwa kuwa na chachu ya ongezeko la kasi ya ukuaji wa uchumi, elimu(sayansi na teknolojia), siasa na ustawi wa  jamii. Ongezeko hilo ndio ishara ya kuwa tuna maamuzi yetu wenyewe kama nchi huru  na tunajitegemea kiuchumi,kisiasa na kiutawala, kielimu kwa maana ya sayansi na teknolojia na kijamii. Je, Ni  kweli tunajitegemea? Au tunaendelea kujikomboa kutoka utumwani? ItaƧhukua muda gani? Kuna mikakati gani ya kukomboa watanganyika wote  kwa maana ya watanzania kwa sasa?
Kama mtanzania najivunia na kuenzi jitihada za waasisi wa  taifa  la  Tanganyika na Tanzania kwa ujumla maana kazi yao ilikuwa ndio mwanzo wa  ukombozi wa  fikra za watu wa  Tanzania.

Mtanzania anayependa maendeleo hato  acha kutamani uongozi wa  serikali kuu na ndogo pamoja na mihimili ya bunge na mahakama kuwa ni huru  na inayotenda haki. Huru  maana yake  isiyoingiliwa kimaamuzi kutoka nje au ndani ya nchi bali  kwa kufuata misingi ya katiba.

Ni makosa makubwa mtanzania kusema tulipata Uhuru Wa bendera, na ukosefu wa  maarifa juu ya kile  tunachokiita tisa Desemba. Nikimnukuu mwanasiasa mwanamke wa kwanza kugombea urais Tanzania Mh. Anna Mghirwa akiwa kwenye harakati za kutapatapa kuhamia CCM hapo Jana kwenye mkutano Wa UWT alisema,"Siasa ya Tanzania inabadilikabadilika" nilivyoelewa ni kwamba alikuwa anajitetea tu, na ukweli ni kwamba kama inabadilika ni vyema na ndio jambo jema. Ila swali litabaki palepale inabadilika kutoka wapi kwenda wapi? Ikiwa inakua ni vyema ila kama inadumaa kwa maslahi ya watu wachache, hilo  ni tatizo.

Ni jukumu letu la  kwanza la  kiuzalendo kupigania Uhuru wa  taifa letu kuanzia fikra na mitazamo tuliyonayo. Hii ni kiwezesha kupata Uhuru Wa kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni, kielimu na kijamii.

Na 
Mwakajila Frank 
Mwandishi
Team Inspiration Inc.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI