UNAWAZO GANI?



Mwanzo wa kila kilichowahi kufanikiwa ni wazo, wazo lililobadilishwa na kuwa kitu halisi. Kabla hujawa na wazo hilo unatakiwa kuwa na picha ya wapi unataka kufika au nini unataka kufanya. Inakuwa bahati kama unapata mtu wa kukusaidia kuona picha yako kubwa kuhusu maisha yako, vinginevyo unatakiwa uone mwenyewe hiyo picha na utengeneze wazo la kukufikisha huko.

Katika ulimwengu huu tunaoishi mawazo yatakayosaidia makundi makubwa ya watu ndio yanayoweza kushinda na kuishi kwa Muda mrefu. 


Wengi wanaoanzisha mawazo huanzia kutoka kiwango cha chini na kuwa na mipango ya kupanda kuelekea juu hadi mawazo yanapowapeleka. Lakini kikwazo kikubwa kwa hili ni kwamba wengi wanaoanzia chini wanashindwa kuinua vichwa kuona FURSA zilizowazunguka kutokana na mawazo waliyonayo kwahiyo wanabaki na mawazo mazuri wakiwa chini. Inatakiwa kukumbuka kuwa mwonekano wa huko chini sio mzuri na unatabia ya kuua tamaa ya mambo makubwa unayoyaona.

Wazo hutambuliwa kama chanzo cha utajiri, mawazo yenye mwanzo usio na faida sana yamekuwa chimbuko la matajiri wakubwa duniani.

Wazo linaweza kuzalisha pato zaidi ya daktari, mwanasheria, mhandisi wakawaida kwasababu yeye itamchukua muda mrefu kujifunza sana ndio apate anachotaka.

Maarifa sahihi yanaweza kuwa kitu cha kuchochea wazo kuendelea mbele, picha juu ya nini anataka kufanya ndio inayoweza kupatanisha maarifa aliyonayo na wazo lake.

wazo huletwa na ubunifu, wazo ndio kitu kikuu na maarifa hupatikana na kutumika baada ya uwepo wa wazo. Unaweza usiwe na elimu kubwa ukapata wazo zuri baada ya kutumia ubunifu kupata picha kubwa inayokuhusu.

Bila ya mawazo duniani tungekuwa bado tupo zama zile za mawe. Mawazo yameathiri kwa sehemu kubwa maisha ya wanadamu duniani na sipati kigugumizi kusema kuwa dunia inaongozwa na watu waliokwisha kufa miaka mingi sana iliyopita. Ndio, waliokufa wengi mawazo yao bado yapo yanaishi duniani, na yanatawala kila kona ya maendeleo tunayoyafanya na mengine yametufunga hata tukashindwa kuwaza mambo mapya.
Kuanzia darasani, mtaani mpaka uwanja wa siasa ni mawazo ya watu. Vip kuhusu imani je? Serikali, biashara na mengine mengi? Utakuja kugundua hata imani ambazo leo watu wanauana kwasababu ya hizo zilikuwa ni wazo tu na likapata kudhihirika na kuwa uhalisia.

Mungu ndio chanzo cha mawazo na akatoa mfano kwa kuonesha wazo linatendekaje. Wazo lake limejificha kwenye neno lake analotamka, maagano anayoweka na watu wake tangu mwanzo wa ulimwengu.

Mawazo yanatabia ya kuibuka na kutoweka na kurudi tena upya kwa muonekano mwingine. Mungu akamuumba mwanadamu na akampa kutawala dunia na vitu vyake vyote. Mwanadamu alipomkosea Mungu ,wazo la Mungu alikuishia hapo liliendelea kujificha ndani ya maagano aliyoweka na vizazi kama Ibrahim (mwanzo 12:1-3), Isaka (mwanzo 17:19), Yakobo ambaye ndio Israel (mwanzo 28:13_22). Hii ni kukuonesha kuwa mawazo yanatabia ya kutoweka na kuibuka huwa hayafi hata mtu akifa yanaendelea kuishi.

Wazo hilo la Mungu la kumpa mwanadamu utawala halikufa licha ya vizazi hivyo kupotea. Vikapita vizazi 42 tangu ibrahimu ( mathayo 1) kupokea wazo hadi kuja kwa Messiah ( Yesu Kristo) duniani kukomboa ulimwengu kwa mara ya kwanza na kufa msalabani kama wazo la Mungu lilivyomtaka. Wazo lilifukiwa katika kipindi cha agano la kale na Mungu hakulifanya siri akazidi kulifungua kwa manabii mbalimbali.

Wazo la Mungu linaishi hata leo kwa wale wanaoamini ( hebrania 9:15) kwamaana Yesu kristo ndiye mbeba maono yaliyotokana na wazo la Mungu hao watu wanaitwa wakristo yaani wapakwa mafuta.

Lengo langu halikuwa kueleza imani, La, bali ni kukuonesha kuwa unatakiwa kuwa na wazo linaloweza kukuzidi umri na kuishi zaidi yako vizazi na vizazi na kusaidia watu wengi.



Leo tunazungumzia demokrasia ambayo ilikuwa wazo la wayunani wa athene lakini hadi leo wazo linaishi. Hata simu unayotumia ilitokana na wazo la mtu Fulani ambaye wazo lake lilitokana na wazo la mtu mwingine. Steve Jobs alileta mageuzi ya teknolojia ya mawasiliano ya simu bila waya, lakini kabla yake kuna mtu anaitwa Martin Copper kabla ya Copper alikuwepo Alexander Graham Bell.

alipokufa Galileo Galilei 1642 ndio mwaka ambao Isaac Newton alizaliwa na wote walitoa mchango mkubwa kwenye kanuni za fizikia hasa mwendo wa viumbe vya duniani na angani.


Siri kubwa ya mafanikio yetu ipo kwenye mawazo yanayotokana na kufikiri kwetu kila siku, unawazo nini na unafikiri nini? Wazo linatoka wapi? Na maswali mengine mengi yakujiuliza unatakiwa kuwa nayo. 

unaweza kuamua dunia iweje kama unawazo lenye nguvu na ukalitendea kazi, kama tunavyoona leo mawazo mengi yakipita duniani kuamua maisha ya watu wengi huenda bila ridhaa yao. nimeandika dunia inaongozwa na watu waliokwisha kufa kwa maana ya kwamba waliacha mawazo makubwa yanayoendesha dunia. 

Tuna watu wachache wenye mawazo makubwa wanaoishi leo nao pia wanaendesha dunia, ukiamua unaweza kuwa mmoja wao au ukawa mpokea mawazo na kuyatendea kazi vyovyote ni sawa.

Mungu ametupa fursa ya kuvumbua mawazo mapya tutumie uwezo wa ndani tulionao kujenga picha ya maisha tunayoyataka kuishi na wazo litakuja, kama ni la Mungu litasimama na kudumu na kuleta mageuzi duniani, vinginevyo litaangushwa.

Frank Mwakajila
mwandishi.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI