TISA DISEMBA NA UHURU WA FIKRA
    " Hakuna  umaskini  mbaya  kama umaskini  wa   fikra " moja ya nukuu za Hayati Mwalimu Nyerere JK. Akimaanisha umaskini unaotokana na fikra za kitumwa, kushindwa au kutopewa fursa ya maamuzi juu ya hatma yako, kuwepo duniani kwa lengo la  kuongeza idadi ya raia  na si  huru  kama wengine.        "Hakuna anayeweza kukutawala bila kuanzia kwenye ufahamu wako" utawala mzuri na makini unaanzia kwenye fahamu yani kukufanya utengeneze fikra ya kuwa mtumwa na uwe  umeridhika na kutumika. Siku  hizi neno zuri ni  Mtumishi( ina  maana sawa na mtumwa wakati mwingine lina maanisha mfuasi).     Uhuru una maana halisi ya kuwa na haki ya maamuzi binafsi bila ya kuingiliwa na mtu  au taifa lingine. Huwezi kufanya maamuzi yako bila kuhusisha fikra. Kwa maana hiyo mwenye Uhuru Wa fikra pekee ndio raia  huru  kweli na si  vinginevyo.    " Mtumwa  hata  akipewa  haki  ya kuamua  atafanya  kama anavyofikiri  Bwana wake."     Uhuru tuliona...