Posts

Showing posts from December 29, 2016

NEW YEAR RESOLUTION DON'T CHANGE YOUR CONFESSION

Image
HamasikaLeo Haujazeeka sana kiasi cha kughahiri malengo yako au kushindwa kuweka malengo mapya. Mambo mengine umekuwa  ukiyapanga na kupangua na kupanga kila mwaka bila mafanikio. Umekutana watu wanaojiita wahamasishaji kama huyu anayeandika na wamekufanya ujione kama hujawahi fanikiwa na kujisikia umechelewa na kukata tamaa. Ukipiga mahesabu ya mwaka 2016 hauoni fanikio la  kukufanya ufarijike na huenda ulipanga vizuri sana. Kuna ugonjwa fulani  wa mtu  kupanga kitu na unapofika muda wa utekelezaji hatekelezi mpaka muda unapita  na kupanga tena na tena, basi unakuwa  mchezo wa kupanga. Unajisikia ukakasi sana pale mwaka unapoisha hujafikia malengo yako au umefikia kwa kiwango hafifu. Wengi huwa tunabadili misimamo na kauli zetu tunapokutana na hali ya kutofikia malengo. Unaweza tumia mbinu hizo zinazoitwa mbinu za mafanikio na husionje hata harufu ya mafanikio na kuishia  kushawishika kukubaliana na hali halisi ya ugumu wa maisha. Takwim...