TEMBEA MBELE




Nilipokuwa nafikiria kuhusu mwezi wa tatu tulioanza leo nikakumbuka kitu kuhusu maana inayofanana na jina la mwezi huu. Mwezi wa tatu kwa kalenda ya Gregorian tunayotumia unaitwa kwa jina March, lenye maana yake kutokana na asili yake. Sikutaka kung’ang’ana na maana yake na asili yake ila nikafikiri kuhusu maana yake kwa lugha ya kimombo. March maana yake ni MWENDO. Tumetembea sana kwaajili ya mwenge, maadhimisho na mambo mengine mengi kama ishara ya kutiana hamasa.

Mara nyingi kwenye matukio ya pamoja yanayogusa maisha ya kila mmoja watu huwa wanaandaa matembezi ya pamoja juu ya swala fulani. Lugha nyepesi wanaita maandamano ya amani, wengine wanasema matembezi kwaajili ya.......... kuna sababu kubwa moja ya msingi inayowafanya watu wafanya matembezi.

Watu hufanya matembezi ili kujenga ufahamu kwa watu wote wanao kerwa na jambo hilohilo kuwa hawakopeke yao, ndio maana maandamano hayo hayana mwaliko. Mtu yeyote anaweza kuungana na kundi la watembezi kufanya wanachofanya kama amenia kuungana bila kuleta vurugu.

Matembezi ya kupinga ukeketaji, matembezi ya kupinga vifo vya albino, utoaji mimba, siku ya kisukari na mambo mengine mengi amabyo kila binadamu anaweza kuguswa nayo.

Dhima yangu sio kukukumbusha ufanya matembezi ya amani, bali ni kukujuza kuwa mwezi huu ni mwezi wako wa KUSONGA MBELE, kwa yote uliyokuwa umepanga kufanya kwa mwaka huu na nina uhakika kuwa umeanza kujiweka sawa tangu mwezi wa kwanza. Hivyo  hatua ya pekee kwa mwezi huu ni kusonga mbele tu.





Ufunuo 22:1-2


 Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
 

Usiwe sababu ya kutokupata matunda kwenye uliyoyapanga kwa kusitasita kusonga mbele kwa ushindi. Ukiwa unawaangalia wafanya kazi wanaokuwa wanafanya matembezi ya mei mosi wakiimba solidarity forever sio kwamba hawana shida ni kujitia morali wa kusonga mbele. Ukitaka kuongeza mwendo wa mambo yako unayofanya lazima uimbe wimbo mmoja kwenye maisha yako yaani uwe na kauli moja ya kufanya jambo sio kuwa kigeugeu.




March up

March for your life


 Frank Mwakajila

Mwandishi 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI