KUWA WEWE

rethink
 KUWA WEWE

umewahi jiuliza unapenda kuwa nani kwenye maisha yako? au umewahi kuulizwa unapenda kuwa nani kwenye maisha yako?, wengi hutoa majibu ya ajira wanazopenda na wengine hufika mbali hata kutaja kampuni wanayopenda kufanyia hiyo ajira. Sio mbaya sana ila ni hafifu inakupima kiasi gani kwenye maisha yako hujawahi fikiri kutawala na kumiliki. Mungu hakuumba watu mashuhuri na wasio mashuhuri aliumba wote sawa na kuwapa uwezo mbalimbali unaotofautiana........
               "tu sawa lakini hatulingani"
Tangu nimefahamu uwezo uliondani yangu sijawahi tamani kuwa flani, nasikitika kwa nini sikufahamu mapema uwezo nilionao. Leo ukiniuliza unataka kuwa nani nitakujibu nataka kuwa MIMI yaani vile nilivyojaaliwa na mwenyezi Mungu kuwa wapekee ndivyo niwe. Usiogope wewe pia una UWEZO.....Uwezo wako unaweza kuwa kwenye vidole vyako kama vile mimi ninavyochapa hili chapisho, unaweza kuwa kwenye miguu kama vile Lionel Messi anavyowashangaza wengi, unaweza kuwa kwenye mikono kama Dr.Benjamin Carson.Sr.

kuna maana nyingi za mafanikio leo tuangalie hii moja niliyojifunza kutoka kwa mwandishi wa THE RICHEST MAN IN  BABYLON, George.S.Clason katika maneno yake ya utangullizi ameandika, " mafanikio ni kutimia kwa jambo kama matokeo ya jitihada zetu na uwezo tulionao". Kutimia, jitihida, uwezo na matokeo ni maneno muhimu kwenye maana hiyo.
JITIHADA;- ni dhamira ya dhati katika kufanya jambo.
KUTIMIA;- ni ukamilifu wa jambo linalifanywa.
MATOKEO;- hali inayoonekana baada ya jambo kukamilika
UWEZO;- ni nguvu kazi inayopelekea jambo linalitakiwa kutimia litimie.



Kimsingi dunia yote hatuwezi tukawa mabilionea au watu washuhuri, lakini tunaweza kuwa angalau wazazi wa watu mashuhuri wajao. Mark zuckerberg mjasiriamali wa mtandao ni tajiri wa tano kwa sasa ulimwenguni akiwa na umri wa miaka 32, wengi tunaweza sema amepata zali la kugundua programu ya kompyuta, la hasha kakuna kitu kinaitwa zali kwenye sayari ya dunia. Mazingira na wazazi wake wamechangia yeye kufika pale alipo kwasababu walitambua UWEZO wake alionao………Matajiri wa Africa hawawezi elezea utajiri wao wazi sifahamu kwanini, ila naamini wao pia wametumia UWEZO wao wa ndani….

Nikisema uwezo wangu au wako ni kwamba vile ulivyojaaliwa kufanya ambavyo hakuna mtu duniani anafanya, nikisema hakuna,ni  hakuna kweli na hajawahi kutokea. Kama wewe ni fundi viatu na ukashona viatu kama kazi ya mikono unayoipenda sio kwasababu usipofanya njaa itakumaliza, hakika utashona kiasi cha kutoweza kufananishwa na mtu yeyote duniani….

Uwezo wako ulionao ndio utakufanya uwe tofauti na wengi sana wanaokuzunguka. Nakataa na ninakusaidia kukataa kuwa tunalingana, anayelingana na wewe hajazaliwa bado, atazaliwa pale utakapokubali kushindwa…kushindwa kutambua uwezo ulionao. Ben carson MD kwenye kitabu chake cha “mikono iliyozawadiwa” ameandika…
                   <sio nini unafanya, ila namna unavyofanya kazi unayofanya ndio unaweza leta utofauti”>…..

Wakati mwingi ninapenda kukaa peke yangu na kuanza kujitathmini mwenyewe nikijiweka kizimbani na kujihoji, kujikosoa na kujikumbusha mikakati. Muda wako wewe na mtu wako wa ndani utakusaida KUJITAMBUA NA KUJIENDELEZA. Kuna watu wanavito vya thamani kwenye miili yao na hata sasa hawajavitambua, inawezekana sauti, hekima, uongozi,mwonekano,elimu na vingine vingi vinaweza kuwa na uwezo. Ni huzuni sana kama hutaweza kutambua uwezo wako mpaka mauti ikufike maana itakuwa hasara kwa ulimwengu wote kupoteza tunu yenye thamani iliyondania yako…………itaendelea

Nukuu yangu:-
“Potential and success are married unless ignorance proclaim divorce”

Frank Mwakajila,
C.E.O,
World Inspiration Inc.
Inspired by God living to the limits of our potential.










Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI