DO ONE THING TODAY.....


DO ONE THING TODAY.......
 (Review of “The One Thing”)
 

MATOKEO YATOFAUTI KATIKA MAISHA YAKO YANATOKEA PALE UNAPOFANYA  TOFAUTI.

Mafanikio yanataka umoja wa malengo yaani kuwa na lengo moja kwa Muda Fulani na kuliwekea mikakati ya kutimia.Unatakiwa kufanya mambo machache kwa matokeo mazuri, na sio mambo mengi yenye matokeo mabovu.
Doing same things over and over and exepecting different result….
          Uchu wako katika kufanya jambo hupelekea mgawanyo wa muda mwingi katika jambo hilo. Hivyo hupelekea matokeo mazuri yatayofanya ufurahie kazi hiyo na kuifanya zaidi na zaidi. Na  uchu zaidi na muda zaidi utawekeza katika kazi hiyo au jambo hilo. Inakuwa mzunguko wa matukio katika maisha.
Watu wengi wanaopoangalia nyuma kwenye safari ya maisha yao mara nyingi mambo hawakuyafanya ndio yanayo wavunja mioyo. Wala yale waliyoyafanya hayawafanyi kujipa moyo sababu ni madogo sana.

Hakikisha kwenye maisha yako unafanya yale yanayofaha haswa yani yenye tija kuliko. Utakapo tambua yale yanayofaa haswa kila kitu kitakwenda sawa, usipotambua yale yanayofaa kitu chochote utaona sawa kukifanya.
Maisha makamilifu yanapimwa kwa njia nyingi njia moja wapo ni kuishi bila lawama au majuto.
KUFANYA MAMBO MAWILI KWA WAKATI MMOJA NI SAWA NA KUTOKUFANYA
             Kanuni ya kufanya jambo ni muunganiko wa kufanya kwa uwezo wako wote pia kufanya jambo hilo vile linavyotakiwa kufanywa.Kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja ni uwongo, mtu huyo huyo ni mchungaji, mwigizaji,mtangazaji wa luninga na redio, mshauri na sahaa,mhamasishaji na bado ni baba wa familia. Kuna mambo mengi atayafanya vile yasivyotakiwa, mara nyingi inakuwa hivyo katika harakati za kutafuta riziki.
                                         MUDA

            Siku ina sekunde 86400 mwanzo niliona chache sana, tangu nilipotambua lengo la kuwa ndani ya muda huo ninaamini hizi ni sekunde nyingi sana kufanya mabadiliko katika maisha yangu. Sio kwamba tuna muda mchache wa kufanya mambo yetu ila ni kwamba tunajisikia kufanya mengi sana katika wakati tulio nao. Siamini kwamba lengo la maisha ni kuwa na furaha, bali ni kutumika, kuwajibika na kujitoa.
Matokeo mazuri na yasiyo ya kawaida, hutokea pale unapojitoa kwa vyote ulivyonavyo, ili kuwa vile unavyotakiwa kuwa. Napenda kusema mara nyingi na wanafunzi wangu nikifundisha“ if you can’t risk the usual, be ready to settle for the ordinary”.

My quote:-
“People who are crazy enough to think they can change the world are the only one who do.”

Mwl: Frank Mwakajila
C.E.O
World Inspiration Inc
“Inspired by God living to the limits of our potentials”

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI