MWEZI WA SITA


MWEZI WA SITA NI WA KUTUMIA MAMLAKA KUMSHINDA SHETANI

Namba sita kwenye biblia inamaanisha udhaifu wa mtu na udhihirisho wa dhambi

27Kwa hiyo Mungu alimwumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimwumba,
mwanaume na mwanamke aliwaumba.
31Mungu akatazama vyote alivyoumba na ilikuwa vizuri sana. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.

SITA NI NAMBA YA MTU
Kwasababu aliumbwa siku ya sita, na inabaki kuwakilisha kutokamilika kwetu. Ikumbukwe kuwa Mungu aliumba Mtu. Mtu bila Mungu atabaki kuwa asiyekamilika. Mungu akampulizia pumzi mtu naye akapata uhai.
MTU HAJAKAMILIKA WALA HAJAWAHI KAMILIKA

 Haijalishi kiasi gani tuna fanya jitihada kujikamilisha kwa nguvu zetu na maarifa, tunabaki kuwa chini ya namba saba namba ya ukamilifu.

Licha ya kuto kamilika Mungu alivyoumba vyote akatazama na kuona vilikuwa ni vizuri sana. Inahitaji uweze kuona kama Mungu anavyokuona ndio utaweza kuona ukamilifu kwa njia ya neema ya Mungu.
MTU ALIUMBIWA KAZI KAMA KUSUDI( A WORK IS ART OF BECOMING A TRUE BEING)
Siku ya sita inaonesha kumalizika kwa kazi ya Mungu yaani uumbaji. Mungu akampa mtu kazi katika bustani ya eden ili kuendeleza tamaduni ya kazi na sio laana kama mtazamo wa wengi.

MTU KUPEWA MAMLAKA YA KUTAWALA KABLA AJAUBWA SIKU YA SITA
26Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale 

juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.’’

Licha ya udhaifu tulionao Mungu ametupa mamlaka ya kutawala. shetani hana utawala bali ana nguvu pekee, nguvu bila utawala uwezi fanya jambo. Utawala una mamlaka ndani yake. Ndio maana TRA hawafanyi biashara yeyote ila wana mamlaka ya fedha ya nchi yote, vivyo hivyo TCRA hawana chombo chochote cha mawasiliano ila wao ndio wanasimamia mawasiliano.

Nyoka aliyemdanganya mtu naye aliumbwa siku ya sita, ila alichokosa ni mamlaka juu ya mtu.

Shetani anatuweza pale tunapojaribu kujisahau na kutumia nguvu, bila mamlaka

SITA NAMBA YA USAWA, USHIRIKIANO NA UPATANISHO
Muujiza wa kwanza wa Yesu ulikuwa wa kubadilisha mitungi ya maji kuwa divai, kwenye sherehe ya DOA. Ndoa inamaanisha upatanisho. 

Inaweza ikawa sababu ya boaz  kumpa ruthu vipimo sita vya shayiri. Ruth 3:15

Kama tunapenda mambo ya kimungu yatokee  kwenye maisha yetu tunatakiwa kukumbuka kuwa hatujakamilika pasipo Mungu. Tukubali kujazwa mpaka juu kabisa kama mitungi ya maji, kama vile divai ilivyokuwa ajabu katika harusi ya kana kadhalika maisha yetu.

My quote:-
And they overcame him by the blood of the Lamb, and by the word of their testimony; and they loved not their lives unto the death.

Written by: Mwakajila F.A
C.E.O
WORLD INSPIRATIONISM INC
’’inspired by God living to the limits of our potential’’

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI