FUNGUO 5 ZA MAAMUZI


  
              Kila mtu ni mfanya maamuzi. Tunategemea taarifa na mbinu za kutuwezesha kufanya hayo maamuzi na hapo ndio maamuzi yanapotofautiana baina yetu. Tunapokwenda mgahawani, orodha ya chakula ndio inayotupa nafasi ya kufanya maamuzi kwa kutupa taarifa sahihi za chakula kilichopo mahali hapo. Orodha hiyo ya chakula inafika mbali kwa kutupa gharama ya kila chakula tukakacho kula, hivyo kuweza kupima gharama ya matumizi yetu kabla ya kutumia. Kufanya jambo lolote ia kunahitaji kufanya maamuzi, kwenye biashara, kazi hadi siasa inahitaji maamuzi ya awali.

Uamuzi unafanyika katika hali ya kutokuwa na uhakika, wakati ujao haujulikani na wakati mwingine wakati uliopita hali yake ni ya makisio tu. Chapisho hili linaweza kukusadia kukupa mbinu za kukusaidia kuhimiza uwezo wako wa kufanya maamuzi katika ulimwengu tulionao ambao mambo mengi hayanauhakika, hubadilika badilika na wakati mwingine hali nyingine zinazoweza jitokeza zisizoweza kuzuilika.

Ongeza chaguzi zako
Kuamua kunatanguliwa na kitendo cha kuchagua kwanza, kabla haujaamua ninauhakika unakuwa na mambo mbele yako na unataka kufanya moja kwanza au moja tu na kuachana na mengine yote. Unachotakiwa ni kuongeza uwanja wa mambo unayoyachagua kabla haujaanza kuyapunguza moja baaada ya linguine. Ukiwa na machagulio mawii tu unakuwa na uwanja mdogo wa kuamua. Ni kweli inafika wakati mambo ya kuchagua yawe machache ndio urahisi unakuja, yatakuwaje machache kabla hayajawa mengi?

Jaribu machagulio yako kabla haujabaki na chaguzi moja.
Chaguzi zako nyingi zitafutie taarifa sahihi kwanza zote kwa usawa, usiwe na upendeleo wa kitu kimoja kwanza kabla ya kuchunguza vyote. Tatizo hili kinawakumba wengi sana kwa kuwa na upendeleo wa machagulio waliyonayo. Unataka kufanya biashara na una mawazo matan ya biashara, kati ya hayo matano tafuta taarifa sahihi kwa usawa juu ya mawazo yote. Mwisho utafikia hatua ya kuamua moja la kufanya au mawili kulingana na ulivyopanga.

Epuka mihemko ya muda mfupi.
Tumia kanuni ya 10/10/10 baada ya dakika 10 utajisikiaje kuhusu maamuzi hayo, vip kuhusu baada ya miezi 10? Na vip kuhusu miaka 10? Epuka kupotezwa katikati ya hisia za muda mfupi zinazokupa mihemko ya muda mfupi na kukuacha ukiwa unajuta. Maamuzi mazuri ni yale ambayo matunda yake yanadumu kwa muda mrefu kufaidisha maisha yako yote.

Jiandae kukosea kufanya maamuzi.
Ni jambo la ajabu kujiandaa kukosea kufanya kitu wakati umefanya kwa uhakika. Mamuzi ni jambo la kuweka uhakika pasipo na uhakika. Tatizo letu wengi tunapokuwa tunafanya maamuzi tunasahau kama mwanzoni yalikuwa makisio ya jambo na kuweka imani zetu zote hapo, sio kila maamuzi mazuri unayofanya lazima yafanikiwe na sio kila maamuzi ambayo hayakufanikiwa hayakuwa mazuri. Hatua za mwanzo zikikosewa kufuatwa hii hatua ya nne lazima itajitokeza. Kukosea maamuzi kunafanya wafanyabiashara wafirisike, wafanyakazi wafukuzwe kazi lakini wote bado wanatakiwa kujiandaa kwa hayo yote.

Kuwa tayari kubadili maamuzi
Ukiwa na kitu unatamani kwenye maisha huwezi shindwa kuwa tayari kubadili maamuzi yako. Kanuni ya shauku+uamuzi×nia=hatma inaeleza wazi kuwa maamuzi ndio yenye uwezekano mkubwa wa kubadilika. Maamuzi ndio yenye uwezo wa kuathiri maisha yako yote yaani hatma yako ikawa sivyo ulivyotegemea.

Msimamo wa kimaamuzi ni muhimu kwa kila mtu kwasababu kila mtu ni mfanya maamuzi. Ufasaha wa maamuzi ndio ufasaha wa mipango yako na ndio hatua za kufanikisha mambo unayofanya. Uwe na uhakika kuwa unafanya maamuzi kwaajili ya maisha yako na maisha yako yatakuwa vile unavyoenda yawe. Mara zote tunavunjika moyo kwasababu tuna matarajio mengi kuhusu maamuzi yetu na yanaokuja tofauti tunashindwa kukubaliana na matokeo, huu usiwe mwisho wa kuendelea kufanya maamuzi sahihi.

Frank mwakajila
Mwandishi.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE WA THAMANI NA TABIA ZAKE 30

KUJIKATAA.KUKATALIWA.KUKATA TAMAA.

UNAWEZAJE KUKOMBOA WAKATI